News
Loading...

Pendezesha manispaa yako, Mh!




Huu ni mtaa wa Dunga.
 Kama uonavyo hapo pichani chini huu ni mtaa wa Dunga maeneo ya Bwawani maeneo ya Kinondoni Msisiri. Tela la kubebea taka limejaa na halijaondolewa kwenda kumwaga taka hizo ili lijazwe hizo zizagaazo hapo mtaani, tatizo hili limekuwa sugu katka maeneo haya kama unakumbuka mdau tarehe 10/12/2010 niliandika makala yenye kichwa "Dampo kati kati ya makazi" na nikaonya juu ya usalama wa afya za watoto wachezao pahala hapo na magonjwa ya milipuko kama kipindipindu na mengine mengi, lakini leo hii tunaona jalala jipya tena maeneo hayo hayo. Na kwa bahati nzuri au mbaya jalala hili linatazamana na nyumba ya diwani wa zamani wa eno hili na pia alipata kuwa meya wa wilaya ya Kinondoni miaka ya nyuma. Nitajaribu kuwaona wahusika nijue nini mpango wao juu ya hili. 
PENDEZESHA MANISPAA YAKO 
 kauli mbiu hii inatekelezwa haswa!

FACEBOOK COMMENT

Share on Google Plus

Connect Mkala26

Usikubali kupitwa na chochote kupitia mtandao huu, kupaya yote haya unahaki ya kuungana nasi sasa, Kuungana nasi BOFYA
FACEBOOK, |INSTAGRAM,
.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :