News
Loading...

Mgema akisifiwa..............



Ilivokuwa tarehe 15/dec/2010

Ilivyo leo tarehe 02/Januari/2010.
Ndugu wadau kama mnakumbuka tarehe 15/Dec/2010 nilitoa makala yenye kichwa cha habari "Mnyonge namnyonga" niliwapongeza sana wahusika kwa kuona umuhimu wa kujenga barabara hiyo na nikawaomba waimalize kabla ya mwaka mpya kwa kuwa kipande chenyewe ni kifupi mno hata robo kilometa hakifiki, ili kupunguza msongamano wa magari katika barabara kubwa zilizo karibu na hiyo. Lakini tangu nipige picha ya mwisho mpaka leo ni wiki mbili na siku kadhaa hapana badiliko lolote na tumeingia mwaka mpya 2011. Sielewi hili linasababishwa na nini. Nitafuatilia na kuwajuza kama nilivoahidi wakati nikiandika kwa mara ya kwanza makala juu ya barabara hii itakayounganisha maeneo ya Mwananyamala Msisiri na Kwa Kopa.

FACEBOOK COMMENT

Share on Google Plus

Connect Mkala26

Usikubali kupitwa na chochote kupitia mtandao huu, kupaya yote haya unahaki ya kuungana nasi sasa, Kuungana nasi BOFYA
FACEBOOK, |INSTAGRAM,
.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :