News
Loading...

H-Mbizo ashuti video ya Mvute mvute!


Tunguri juu ya tunguri
Msanii wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo Flava Hamisi Mbizo aka H-Mbizo hatimaye leo hii jumamosi ameanza kuchukua picha za video ya wimbo wake mpya Mvute mvute, Hmbizo ambaye amewahi kutamba na nyimbo kama Mchumba na Kunguru alipotea katika anga la muziki huo wa Flava za Bongo ameibuka upya na wimbo huo Mvute mvute ambao anamzungumzia msichana anayempenda lakini kila akimtokea mrembo huyo amekuwa akimpiga na chini kiasi kwamba akaamua amuendee kwa mganga wa kienyeji  ili amtie ujinga aweze kumkubali yeye. Katika video hiyo amemshirikisha pia mkali wa vichekesho Bambo ambaye ndiye anacheza kama mkware anayeamua kumroga binti wa watu Samia baada ya kumkataa Pia sehemu ya mganga inachezwa na msanii wa maigizo kwa jina Ndemele, yeye huyu ni msanii anayeigiza kama mganga wa kienyeji hivyo basi ili kujenga uhalisia ana kila kitu ambacho mganga wa kweli wa kienyeji huwa anvyo navyo ni kuanzia noti zamani mpaka tunguri za aina mbali mbali. Jionee mwenyewe pichani. HMbizo alipoulizwa anafanya video na kampuni gani bado hakuwa tayari kuitaja ila alisema nawaomba mvute subira baada ya siku tano hivi tutajua nani atakuwa ndiye liyeifanya video hii ya Mvut mvute.
Hiki ndicho kilinge cha bwana Ndemele.
Hii ni shilingi ishirini nyekundu na yenye picha  rais mstaafu
Shilingi mia moja ya noti nyekundu.

Hii ni sh ilingi ishirini ya miaka ya mwanzoni ya uhuru.
Hawa na Samia.
Hawa, Bambo na Samia baada ya kumaliza shooting.
Kutoka kushoto ni Hawa, Bambo, Samia na HMbizo.
Samia, ndiye mrembo anayemdatisha Bambo.

FACEBOOK COMMENT

Share on Google Plus

Connect Mkala26

Usikubali kupitwa na chochote kupitia mtandao huu, kupaya yote haya unahaki ya kuungana nasi sasa, Kuungana nasi BOFYA
FACEBOOK, |INSTAGRAM,
.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :