Huu ndio songamano wa magari uliotokea eneola ajali na kusababisha kusimama kwa safari pande zote.
Habari ambazo hazijathibitishwa usahihi wake zinaeleza kuwa jana majira ya alfajiri karibu na daraja la Wami upande wa Chalinze palitokea ajali mbaya ambapo inasemekana watu watatu walipoteza maisha kufuatia ajali hiyo. Kibaya zaidi kila dereva aliyepita hapo alitaka aendelelee na safari yake bila kufuata sheria za usalama barabarani, jambo ambalo lilisababisha msongamano mkubwa na hatimaye kukawa hakuna gari iliyoweza kupita hapo kwa muda saa kadhaa.
Lori la mizigo likiwa limepinduka karibu na maeneo ya daraja la wami upande wa Chalinze.
0 comments :
Post a Comment