Joseph Shamba akijuliwa hali na Mh Rais Kikwete Muhimbili jijini Dar.
Msanii wa vichekesho Joseph Shamba aka Vengu(28) wa kundi la Ze origino komedi amelazwa katika hospitali ya taifa Muhimbili kwa wiki kadhaa sasa. Haikuweza kufahamika mara moja anasumbuliwa na maradhi gani lakini ni dhahiri kuwa hali yake si nzuri kama ioneshavyo pichani alipotembelewa na Mh Rais Kikwete hivi karibuni. Vengu ni maarufu kwa uigizaji wa viongozi wa serikali na wale wa upinzani hasa Mh Augustine Mrema wa TLP. Nawaomba wa Tanzania wote tumuombee Vengu apate nafuu haraka ili arudi katika shughuli zake za kila siku kama hapo awali.
0 comments :
Post a Comment