News
Loading...

Tigo mnatukamua mpaka maji?


Mtandao maarufu wa simu za mkononi nchini Tigo jana umenifanyia kitu mbaya mara 2. Nilipoanza kutuma msg za Pasaka kwa ndugu jamaa na marafiki nikapata sms toka tiGO ikisema Endelea kutuma sms.Ukishatuma sms 10 za kulipia, subiri ili uweze kupata uthibitisho ili uweze kutuma sms bure siku nzima. Kitokeo cha hapo nikasubiri nikaona sipati uthibitisho na mimi nahitaji kutuma sms matokeo yake nikajikuta nimetuma sms 25 bila kupata uthibitisho ambazo gharama yake ni Tsh 1250. Kama hilo halikutosha kuwa zawadi nono ya kwangu PASAKA nikatumiwa salio la Tsh 5000 na rafiki yangu. Salio hilo lilipoingia katika simu yangu likaja na sms Ndugu mteja umepokea Tsh 5000 toka kwa namba ................ umekatwa sh 150 kama ada ya hamisho hilo la pesa. Sasa ndugu zangu hebu niambienia aliyenitumia kakatwa na mimi mpokeajji nakatwa, sasa huku ni wapi tunapoelekea? TCCRA wawaangalie hawa tiGO jamani wasije wakatatukamua mpaka maji!

FACEBOOK COMMENT

Share on Google Plus

Connect Mkala26

Usikubali kupitwa na chochote kupitia mtandao huu, kupaya yote haya unahaki ya kuungana nasi sasa, Kuungana nasi BOFYA
FACEBOOK, |INSTAGRAM,
.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :