News
Loading...

Miss Tabora kupatikana leo!


Kile kindumbwe ndumbwe cha kumsaka Miss Tabora 2011 kilichokuwa kikisubirirwa kwa hamu kinatarajiwa kufanyika leo saa 2 usiku katika ukumbi wa New Royal Garden, akithibitisha hayo muandaaji wa Miss Tabora Bw Mgalula Fundikira alisema jana katika mkutano na waandishi wa habari kuwa zawadi za washindi zitakuwa kama ifuatavyo;
  

1. Dell Desktop Computer ya laki sita na kozi ya Musoma utalii college ya laki tatu.
2. Dell laptop computer ya laki tano na kozi ya Musoma Utalli college ya laki mbili
3. Subwoofer na Dvd player ya laki mbili kozi ya laki moja unusu.
Na wasiriki wa nne mpaka wa kumi watapatiwa kifuta jasho cha sh laki moja kila mmoja.

Vile katika kusindikiza shindano hilo patakuwa na burudani murua toka wasanii wa Tht Amini, Nash D. Pia watakuwepo Steve RnB na Hmbizo mtoto wa Isevya. Mgeni wa heshima atakuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw Abeid Mwinyimsa. Warembo hao wamekua wakifundwa na Miss Tabora wa 2010 ambaye atamaliza muda wake leo hii atakapomkabidhi  Miss Tabora mpya taji hilo.

FACEBOOK COMMENT

Share on Google Plus

Connect Mkala26

Usikubali kupitwa na chochote kupitia mtandao huu, kupaya yote haya unahaki ya kuungana nasi sasa, Kuungana nasi BOFYA
FACEBOOK, |INSTAGRAM,
.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :